Contacts

Wednesday, June 5, 2013

MAELFU WAUAGA MWILI WA MANGWEHA

Maelfu ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam na vitongoji vyake wamekusanyika katika Viwanja vya Leaders Kinondoni kumuaga msanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya, Albert Kenneth Mangweha 'Ngwair' aliyefariki dunia ghafla Mei 28 mwaka huu huko nchini Afrika Kusini. Mwili wa marehemu Mangweha baada ya kuaga utasafirishwa kwenda mkoani Morogoro tayari kwa mazishi yatakayofanyika kesho.

No comments:

Post a Comment