Contacts

Saturday, June 29, 2013

HUU NI UJINGA MTAKATIFU WATANZANIA EBU TUAMKE YA NINI SASA YEYE KUJA BORA YA UJIO WA CLINTON NA BUSH BASI KUNA KITU


FBI KUCHUJA VIONGOZI WATAKAO MPOKEA NA KUONANA NA OBAMA

Dar es Salaam. Wakati magari 150 ya msafara wa ziara ya Rais Barack Obama yamewasili nchini, majina ya mawaziri wa Tanzania yatakayoruhusiwa kumpokea kiongozi huyo kuchujwa na makachero wa FBI.

Mkurugenzi wa Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere, Moses Malaki aliliambia gazeti hili jana kuwa matayarisho ya ujio wa Rais huyo ni kabambe na hayajawahi kutokea katika historia ya Tanzania.

Pia alisema shughuli za kumpokea Rais Obama, anayetarajiwa kutua Jumatatu saa 8:40 mchana, zitaanza asub

uhi kwa maofisa wa Marekani kushika majukumu yote katika uwanja huo, ikiwemo kuongoza ndege, ukaguzi wa abiria na mizigo, kwa maana wafanyakazi wa uwanja huo kuwa likizo kwa siku mbili.

“Wamesema kuwa wao watasimamia kila kitu kuanzia wageni watakaoingia na kutoka na wataamua nani aingie na kutoka,” alisema Malaki. Imebainika kuwa hata idadi ya maofisa wa Tanzania wakiwemo viongozi watakaompokea pia itapangwa na Wamarekani wenyewe.


“Wenyewe wana orodha yao na wanajua nani atakuwepo au hatakiwi kuwepo katika kundi la wageni watakaompokea Rais Obama,” alisema na kuongeza:


“Nilimuuliza Ofisa Usalama wa Marekani iwapo nitaweza kumwona Rais Obama, akaniambia: Utamwona ukibahatika kuwepo kwenye orodha.”


Waziri wa Sheria na Katiba, Mathias Chikawe naye alikiri kuwa mawaziri wanaotakiwa kuwepo katika msafara wa kumpokea Rais Obama ni wachache watakaochaguliwa tu na Wamarekani, baada ya kuyapitia na kuyachunguza majina hayo kwanza kabla ya kuyakubali.


“Hii sijawahi kuiona, hata sisi wenyewe tunateuliwa na wakishayapitia wataamua, nani aende au 

Friday, June 28, 2013

LUNDENGA MSHIRIKI WA UREMBO JUKWAANII!!!!



Na Dustan Shekidele, Morogoro
MWENYEKITI wa Kamati ya Mashindano ya Miss Tanzania, Hashimu Lundenga Jumamosi iliyopita alimtimua mshiriki wa shindano la Redd’s Miss Morogoro 2013, Saphina Chumba (20) jukwaani wakati shindano hilo lilipokuwa likiendelea.
Mrembo Saphina Chumba akiwa jukwaani na vazi lililomtia matatani.
Tukio hilo lilitokea Jumamosi iliyopita katika Ukumbi wa Hoteli ya Kitalii ya Nashera mjini hapa wakati mrembo huyo alipokuwa akiwania kuvaa taji la mkoa huo.
Kisa cha mrembo huyo aliyevalia namba 5 kutimuliwa ni kukiuka maadili na kanuni za mashindano hayo kwa kuvaa nusu utupu mbele ya mgeni rasmi ambaye alikuwa Mbunge wa Kilosa, Mustapha Mkulo na mbele ya Kamati nzima ya Miss Tanzania.
Saphina kabla ya kugeuka na kuonyesha makalio.
Baada ya kuona jinsi alivyovaa, Lundenga na kamati yake walikubaliana kumtimua mshiriki huyo kwa kumwita Jaji Mkuu wa shindano, Alex Niktasi na kumtaka amuondoe haraka.
Hashimu Lundenga.
Mbali na Chumba, pia jaji alimtimu mrembo mwingine aliyevalia namba 8, Neema Joel (20) kutokana na kushiriki shindano  hilo mara mbili mwaka huu, inadaiwa mara ya kwanza alishiriki mkoani Arusha.
Lundenga alipohojiwa na mwandishi wetu alisema kamati yake inataka kuendeleza nidhamu tangu ngazi ya chini, hivyo hawawezi kuruhusu utovu wa nidhamu.

Thursday, June 27, 2013

ZIARA YA OBAMA SENEGAL


PICHA MBALI MBALI YA KILICHOJIRI HUKO SENEGAL KATIKA MAPOKEZI YA OBAMA

obama-senegal
obama-senegal

CELEBRETIES WENYE MVUTO NA KUINGIZA KIPATO KIKUBWA DUNIANI

Katika orodha hii nafasi ya kwanza kabisa anashikilia mwanamama Oprah, na hii ni kutokana na nguvu yake kubwa katika Televisheni pamoja na mitandao ya kijamii, na pia anamiliki wa Cable Network kubwa kabisa ya Oprah, na kwenye rekodi inaonyesha kuwa kati ya mwezi June 2012 na June 2013 amejivunia kiasi cha dola milioni 77, sawa na shilingi 124,008,500,000 za kitanzania .
Katika nafasi ya pili anasimama, Lady Gaga ambaye ana nyota ya kupendwa na watu kutoka kona zote za dunia, akiwa anaongoza kufuatwa katika social networks hasa kutokana na muonekano wake wa kitofauti zaidi na Uwezo kimuziki, licha ya kuwa nnje ya stage kwa muda akiwa anapona uparesheni ya hips, ameweza kujivunia dola milioni 80, sawa na pesa za kitanzania, shilingi 128,840,000,000 katika kipindi cha mwaka jana mpaka mwaka huu. 









Katika nafasi ya tatu anasimama TV/Film Director/Producer maarufu Steven Spielberg ambaye yupo nafasi ya juu kabisa na anaheshimika katika fani hiyo akiwa ni mtu mzima mwenye umri wa miaka 59, Huyu kwa mwaka amejitengenezea dola milioni 100, sawa na shilingi 161,050,000,000 za kitanzania.

                       

Katika nafasi inayofuata anasiamama mwanadada Beyonce ambaye mafanikio yake yanafahamika kote, akiwa amejivunia dola milioni 53, sawa na shilingi 85,356,500,000 za kitanzania.
Pia kuna mkongwe Madonna katika nafasi ya tano, akiwa ametengeneza dola milioni 125, sawa na shilingi 201,312,500,000 za kitanzania. 

Nafasi ya sina inashikiliwa na Taylor Swift, dola milioni 55, sawa na shilingi za kibongo 88,577,500,000.
Nafasi inayofuata inakamatwa na Jon Bon Jovi, dola 79, sawa na shilingi za bongo 127,229,500,000.
Nafasi ya saba inashikiliwa na mwanamichezo wa Tennis, Roger Federer ambaye anashikilia dili nono na makampuni makubwa mbalimbali hasa yale yanayofanya biashara ya vifaa vya michezo, dola milioni 71, pesa za madafu 114,345,500,000.
Nafasi inayofuata inashikiliwa na mwanamuziki kinda, Justin Bieber, dola milioni 85, zinazolingana na pesa za kibongo 93,409,000,000.


Na katika nafasi ya 10 yupo mtangazaji mkali kabisa wa TV, Ellen DeGeneres, huyu akiwa na dola milioni 83 ndani ya mwaka mmoja, sawa na shilingi 85,356,500,000 za Tanzania.
#Vigezo vya Forbes katika orodha hii vimezingatia mapato waliyoingiza wasanii hawa kutoka mwezi Juni mwaka jana mpaka mwaka huu, na pia namba ya watu ambao wanawatazama na kuwafuatilia kwa karibu.

Wednesday, June 26, 2013

THIS IS WHO I AM































































 THE SECRET BEHIND THIS IS MY MUM PLUS MY ONLY ONE LITTLE KESSY LUV THEM SO MUCH 

Monday, June 24, 2013

HIKI KILIMTOA P,DIDDY KWENYE UMASIKINI


HIKI NDICHO KINAMFANYA P.DIDDY KUWA MWANA HIP-HOP MWENYE MSHIKO MREFU DUNIA

Kwa mujibu wa Kampuni ya marekani inayochunguza mapato ya wasanii
 dunia kote,hivi karibuni walitoa
mustakabari kwa upande wa Hip-Hop na kumzungumzia Mwana Hip-Hop 

Nguli Sean Carter P.Diddy...

HIII NDO BONGO BANA UMEGUNDUA NINI KWENYE HII PICTURE

SOMO KWA VIONGOZI WETU WENYE NYADHIFA MBALI MBALI

NIONAVYO MIMI VIONGOZI WETU WAJIFUNZE KITU HAPA
Rais wa club ya Ac millan ya Italia na Waziri mkuu Silvio Berlusconi amehukumiwa kifungo cha miaka 7 jela kwa makosa mawili tofauti.Kwanza ni kitendo chake cha kufanya mapenzi na binti anayedaiwa kuwa na miaka 17 wakati yeye ana miaka 76.
Tukio hilo ambalo lilitokea mwaka 2010,nilimtimtia matattizoni mkuu huyu baada ya kuhesabiwa kuwa ni ubakaji kwa binti huyo ambaye ni changudoa mwenye asili ya Morocco.
Silvio pia amekutwa na makosa kwenye tuhuma za rushwa ambazo zinamuandana katika kipindi ambacho amekuwa waziri mkuu.Huyu ndo binti aliyemtoa udenda mzee mzima.

MWANAMKE HUYU NOMA!!


MWANAMKE mkazi wa kijiji cha Ikandamoyo, wilayani Katavi, Veronica Saleh ‘Mama Kaela’ (50), amefanya uamuzi adimu wa kuolewa na wanaume wawili ambao anaishi nao kijijini hapo.

Kijiji hicho kipo umbali wa takribani kilometa 30 kutoka mjini hapa katika Jimbo la Katavi linalowakilishwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Pamoja na ndoa hiyo iliyowezeshwa na mume mkubwa kukubali kuishi na mume mdogo, imeelezwa kuwa mwanamke huyo ndiye ‘aliyewaoa’ wanaume hao kwa zaidi ya miaka saba sasa, huku akiwa na amri kuu katika nyumba, kama ilivyo katika ndoa za kawaida.

Wanaume hao ni Paulo Sabuni ‘Baba Kaela’ (60) ambaye ndiye mume mkubwa na Arcado Mlele (45) ambaye ni mume mdogo.

Taarifa za kuwapo kwa ndoa hiyo ya aina yake, ziliifikia Globu ya Jamii na kufanyiwa uchunguzi kwa zaidi ya wiki tatu, na hatimaye katikati ya wiki hii, wahusika walikubali wao wenyewe kuzungumzia suala hilo. Kwa mujibu wa maelezo ya mwanamke huyo ambaye alionekana kuwa msemaji wa familia hiyo, yeye na mumewe mkubwa, walifika kijijini hapo miaka 24 iliyopita, wakitoka kijiji cha Usumbwa mpakani mwa Chunya, Mbeya na Tabora.

Wakiwa kijijini hapo mume wake aliendelea kufanya kazi ya ukulima wakati yeye mama (Veronica), pamoja na kilimo hujihusisha na upishi na uuzaji wa pombe ya kienyeji iitwayo kayoga.

Mwanamke huyo ambaye amesema ana watoto wanne, Alfred (20), binti mwenye miaka 16 (ambaye ameolewa) na wengine wawili wa kiume, mmoja akisoma darasa la sita na mdogo ana miaka saba, amesema hana shida na waume wake.

Ingawa wanandoa hao walizungumza kwa hadhari, majirani walikiri kuwa mwanamke huyo anaishi na wanaume hao wawili kwa amani na kwamba mwanamke huyo ndiye mwenye sauti na si waume zake.

“Si siri tena sasa, tumeshawazoea, kwani wanaishi kwa amani ila yule mume mdogo anaishi kwenye nyumba aliyoachiwa na marehemu baba yake, lakini anashinda kwa mume mkubwa, ambapo inajulikana kijijini hapa kuwa ni nyumba kubwa. “Basi pale ni mambo yote, kula na kunywa, mama huyu amewapangia zamu wanaume hao kama afanyavyo mume mwenye wake wengi. 

Ama kweli ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni,” alisema mkazi mmoja kwa masharti ya jina lake kutoandikwa gazetini. Ilielezwa, kwamba wanaume hao wana akili timamu na hawatumii kilevi cha pombe kama ilivyo kwa mke wao.

Hata hivyo, mume mkubwa anapewa sifa za upole tofauti na mume mdogo anayetajwa kuwa mkorofi kiasi cha mara kadhaa kumchapa makofi mkewe anapomuudhi.

Majirani wanadai kwamba Mama Kaela na mumewe Paulo, walipofika kijijini hapo, walipokewa na kuishi maisha ya kawaida, lakini baadaye mama huyo alianza kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Arcado, ambaye naye alilazimika kuachana na mkewe wa ndoa anayefahamika kijijini hapo kwa jina la Mama Pere.

Ilielezwa na mashuhuda hao kwamba mume mkubwa alipobaini uhusiano huo, alikuja juu, lakini mwanamke huyo inadaiwa alimweleza mumewe huyo, atake asitake lazima wataishi wawili, vinginevyo ataachana naye, ndipo mume mkubwa alipokubali kuishi na mume mwenza.

Katika maisha ya kawaida katika familia hiyo, inaelezwa kwamba katika baadhi ya siku ikitokea kuwa mama huyo amechoka kupika, mume mdogo huchukua jukumu la kupika na kumwandalia chakula na maji ya kuoga mume mkubwa.

“Lakini mara nyingi kwa mfano, ikiwa ni zamu ya mama huyo kulala kwa mumewe mkubwa, basi humfulia nguo zake kisha anakwenda kwa mumewe mdogo nako anamfulia nguo.

“Ndivyo wanavyoishi, nasi sasa tumewazoea ila yule mama ni mkali na ana sauti pale kwake kwa wanaume wale ila tunaona kama ana wivu sana kwa huyu mdogo ambaye naye pia ana wivu kwa mkewe huyo, labda anahofia kuwa mama huyo anaweza kuongeza mwanamume mwingine,” anasema mmoja wa majirani hao.

Hakuna mazuri yasiyokuwa na machungu, japo familia hiyo inaelezwa kuwa na amani, mtoto wao mdogo nusura avuruge uhusiano wa wanandoa hao, baada ya kuibuka mzozo wakati wa maandalizi ya ubatizo wake.

Kwa sababu anazojua mama, ingawa inafahamika kuwa wote ni watoto wa mume mkubwa, mke huyo katika hati za ubatizo aliandikisha ubini wa mtoto huyo kuwa ni Mlele (akimaanisha kuwa mtoto wa mume mdogo), lakini mume mkubwa aliweka pingamizi kanisani akidai yeye ndiye baba halali wa mtoto huyo.

Kwa mujibu wa mwanamke huyo, yeye na Arcado ni waumini wa madhehebu ya Katoliki wakati Paulo ni Mpentekoste. Madai ya mzozo wa uhalali wa `ubaba’ wa mtoto huyo, yalithibitishwa na baadhi ya wakazi wa kijiji hicho, akiwamo mwalimu wa dini wa Kigango cha Kanisa Katoliki Uruira, Mashaka Abel. Walisema miaka sita iliyopita, mtoto huyo akiwa na umri wa mwaka mmoja, alifanyiwa taratibu za ubatizo, lakini ilishindikana, kutokana na wanaume hao, kila mmoja kudai ndiye baba mzazi wa mtoto.

“Lilikuwa jambo la kustaajabisha sana, kwani familia hiyo ilifanya maandalizi yote ya sherehe ya ubatizo wa mtoto huyo, lakini siku hiyo kanisani wakati huo ilikuwa ni kigango cha Katumba ambacho sasa ni Uruira, sakata lilianzia pale Padri alipomwuliza mama wa mtoto huyo ubini wa mtoto naye akasema ni Mlele.

“Hapo ndipo mume mkubwa alipopinga na kudai kuwa mtoto yule si wa Arcado bali wake na yeye ndiye baba halali. Padri hakuamini, aliuliza tena na tena na majibu yakawa ni yale yale, ndipo ubatizo ukashindikana,” alisema Katekista Abel.

Kazi ya kutafuta undani wa ndoa hiyo haikuwa rahisi kutokana na mazingira ya woga na usiri uliokusudiwa kubaki, ambapo awali mama alisema kwamba mume wake ni Paulo pekee japo siku ambayo mwandishi wa habari hizi alifika kijijini hapo na baadaye nyumbani kwa wanandoa hao na kumkuta mume mdogo (Arcado akimsaidia mkewe kukoroga pombe. Awali katika utambulisho, walidai kuwa ni mtu na mdogo wake na kusita kuzungumzia maisha yao ya kifamilia.

Mke wao ambaye alionekana wazi kuwa ni msemaji mkuu alifoka na kuja juu, akidai kuwa hayuko tayari kuzungumzia uhusiano wake na wanaume hao wawili, ingawa alikiri kuwa wanaishi pamoja.

"Kwa hiyo umefunga safari yote hii kutoka huko ulikotoka ili uje kwangu mie Veronica … nasema sitaki kabisa mtu kuja hapa na kutaka kunivurugia mpangilio wa maisha yangu, kwanza nani alikueleza hayo, wambea wakubwa hao yanawahusu nini watu hao?” alihoji.

“Mie mume wangu ni huyu Paulo basi … sasa leo umeniachia vurugu ndani ya nyumba nitapigwa na huyo mume wangu Paulo, kwani mmenishikisha ugoni?” alifoka Mama Kaela. Hata hivyo, mume mkubwa alidai kuwa hatamwadhibu mkewe huyo na kwamba wataendelea kuishi pamoja na mdogo wake Arcado kwa amani. Hata hivyo, akina mama wengi kijijini hapo wanalaani kitendo cha mama huyo kuishi na wanaume wawili ambapo waliomba uongozi wa Kanisa uingilie kati, ili mama huyo aweze kufunga ndoa na mume mmoja.

Lakini kwa upande mwingine, baadhi walimpongeza mwanamke huyo wakidai kuwa kitendo hicho ni cha kijasiri kwa mwanamke, kumudu kuishi na wanaume wawili na kuwa na mamlaka juu yao.

UMALAYA WA SINZA KUANZIA BAMAGA MPAKA MAPAMBANO


NI hakika ‘mtaa wa ngono’ umefumuliwa! Sakata hilo lilijiri saa tisa usiku, Ijumaa iliyopita, Barabara ya Shekilango, kuanzia Bamaga hadi Sinza Mori jijini Dar eneo ambalo makahaba wameligeuza chumbani, Operesheni Fichua Maovu ‘OFM’.
KWA NINI MTAA UFUMULIWE?
Kwa mujibu wa takwimu za kiserikali, eneo hilo
(kuanzia Bamaga hadi Sinza Mori) limekubuhu kwa wasichana kujiuza nyakati za usiku huku makao yao makuu yakiwa eneo la Afrika Sana hasa pembezoni mwa Corner Bar.
Mmoja wa viongozi wa serikali ya mtaa ya eneo hilo ambaye aliomba jina lake lisiandikwe  alisema:
“Tumejitahidi sana kushirikiana na polisi ili kutokomeza ukahaba eneo hilo lakini wapi! Hawa mabinti ni wabishi, mbaya zaidi wamelifanya eneo hili kuwa la ngono.
“Watoto wetu wanapita usiku pale wanawaona wanavyofanya, wanatuharibia kizazi kijacho, kama wao wamejishindwa wasiwaambukize wengine.”
TIMU ILIYOENDESHA OPERESHENI
Siku ya tukio, saa tisa usiku,  askari wa ulinzi shirikishi walijipanga kwa ajili ya kuufumua mtaa huo huku wakiwa na tahadhari kufuatia habari za kiintelijensia kudai kuwa, makahaba hao walipanga kuua mtu punde watakapovamiwa.
Askari hao wakiwa kwenye doria ya kila usiku, waliwavamia makahaba hao eneo lenye majani madogo katikati ya Afrika Sana na Mapambano upande wa yadi ya Mwanamboka wakiwa na wateja wao wakifanya ngono hadharani.
NUSURA DAMU IMWAGIKE
Katika hali iliyoonesha makahaba wamejiimarisha kwa ulinzi siku hizi, wakati wa zoezi hilo, machangu hao sanjari na vibaka  wanaowaunga mkono wakisemekana ni ‘walinzi’ wao, waliokota mawe na kuwarushia askari hao hali iliyozua tafrani zaidi.
Ndipo piga nikupige ilipozuka ambapo askari walionesha umahiri wao wa kupambana na wahalifu kwa kuwadhibiti kwa vichapo vya hapa na pale na kufanikiwa kuwaweka wengi chini ya ulinzi.
Kuona hivyo, baadhi ya makahaba na wateja wao walifanikiwa kuwachoropoka askari bila nguo na kutokomea gizani hivyo kulifanya eneo hilo kuwa jeupe.
WENGINE WAKIMBIA NA KUACHA NGUO ZA NDANI
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, baadhi ya makahaba waliokimbia walijikuta wakiacha kwenye majani nguo zao za ndani na kuzua maswali kwamba ni kwa nini hawakuwa wamezivaa!
“Jamani hizi si nguo zao za ndani? Ina maana wakiwa kazini hawavai siyo? Wanakuwa tayaritayari kwa kazi? Jamani!” alisema kwa mshangao mkubwa mmoja wa askari hao.
MAKAHABA WALIONASWA WALONGA
Licha ya kuwa chini ya ulinzi mkali, baadhi ya makahaba walionaswa walikuwa wakiwalalamikia askari hao kwamba wanawafuatafuata wakati kila mtu siku hizi anaangalia atakulaje!
“Mnatuonea bure, nyie mnakula kivyenu na sisi mngetuacha tule kivyetu, hao watoto wenu mnaosema tunawaharibu usiku huu wao wanatokea wapi na wanakwenda wapi?” alisikika akisema kahaba mmoja aliyekuwa mtata kuwekwa chini ya ulinzi.
Mwingine akadakia: Kama mnataka tuwape uroda si mseme, mnatukamata kila siku kwani tunawatibulia nini majumbani mwenu? Lini tumekuja kuwaghasi wakati mmelala na wake zenu?”
Uchunguzi wa kawaida ulibaini kuwa muda rasmi wa makahaba hao kuwasili eneo la Corner Bar ili kuanza ‘kazi’ ni saa mbili usiku japokuwa wapo wanaoripoti mapema na kufanya biashara hiyo kwa wizi kulingana na wateja wenye ‘kiu’ nyakati hizo.

AHADI YA MAKAHABA
Licha ya kuwa chini ya ulinzi, makahaba hao waliahidi endapo watapelekwa polisi na kutoka watarejea eneo hilo kujiuza kwani ndiyo ajira inayowafanya waendelee kuishi katika Jiji la Dar es Salaam, kusomesha watoto vijijini kwao na kuwasaidia wazazi wao mahitaji mbalimbali.
“Hata kama mtatupeleka polisi, tutarudi tu hapa, sisi tunasomesha watoto, tunasaidia wazazi wetu vijijini, pia tunaishi Dar kwa sababu ya kipato hiki cha kuuza miili yetu, acheni hizo,” mmoja wa makahaba hao alisema bila kumung’unya maneno.

MWENYEJI WA MTAA ANENA
Akizungumza na paparazi wetu eneo la tukio, mkazi mmoja wa eneo hilo ambaye pia ni askari wa ulinzi shirikishi alisema:
“Kufuatia vitendo hivi kushamiri hapa mtaani hadi kufikia hatua ya makahaba na wateja wao kufanya ngono hadharani kama wanyama, tuliamua kukimbilia polisi kutoa taarifa, kwa hiyo tuna baraka za serikali za kuwatokomeza hawa machangu.”

NDIYO DAWA?
Mapaparazi wa Global Publishers wana uzoefu na makahaba wa mtaa huo unaoanzia Bamaga hadi Sinza Mori, ni wagumu kubadilika.
Mara kadhaa, OFM imekuwa ikiwafumua makahaba hao lakini siku inayofuata wanarudi tena na kupiga kambi kama hakuna tukio lililotokea jana yake!
OFM waliondoka eneo la tukio na kuwaacha askari hao na ‘watuhumiwa’ wao wakisubiri namna ya kufika kwenye Kituo cha Polisi Kijitonyama ‘Mabatini’, Dar kwa hatua zaidi za kisheria.

Friday, June 21, 2013

KWA MTAZAMO WANGU

NIONAVYO MIMI BUS LA TORRES SIPANDI
Kwenye michuano ya mataifa ya ulaya,TORRES kama masihara aliweza kunyakuwa kiatu cha mfungaji bora na hii hii style yake ya kimagumashi.Mechi nyingi alitokea bechi na bila jasho aliweza kupasia nyavu.
Jana naona tena kaokota WALLET kariakoo baada ya kuwafunga wale DJIBOUT ya Australia TAHITI goli 4 peke yake.Hongera EL NINO lakini hata kama mpira ni magoli bado,Torres hajanishawishi.
kazaliwa 1984 bado naamini anauwezo wa kurudi kwenye form na kuendelea kutamba kama alivyokuwa na Atletico Madrid na Liverpool.Kwa hali hii kama atapata magoli mengine mawili ya kimagumashi,ataibuka tena mfungaji bora.
kwa namna anavyocheza siku hizi,hata kama jana Torres angefunga magoli yote 10,bado ingekuwa ngumu kusema kwamba FERNANDO TORRES is back.Nasikitika kuona tunapata mafungaji bora ambao wenyewe sio bora.

Wednesday, June 19, 2013

SI KWELI KABISA KUHUSU KIFO CHA SAIDA KAROLI

TAARIFA ZA KUFARIKI MWANAMZIKI SAIDA KALORI ZAKANUSHWA

Siku ya jana kumekuwa na uvumi kuhusu mwaimbaji 
wa nyimbo za asili bi Saida Kalori zikisema kuwa
 amefari baada ya boti aliyokuwa akisafilia
 kuzama,lakini taarifa tulizozipata kutoka kwa
 mwandishi Neville meena

Monday, June 17, 2013

MBUNGE NINAYE MTARAJIA KWA KIBAHA AKIPEWA FURSA ANAWEZA

anaitwa Jimmy Mrema chini hapa ndo wasifu wake.

Work and Education

Friday, June 7, 2013

M2 P NAE ALIKUWEPO MSIBANI ALILIA KWA UCHUNGU SANA

PICHA ZA M 2 THE P AKILIA KWA UCHUNGU WAKATI WA KUMUAGA ALBERT NGWEA MOROGORO MCHANA HUU


M2  THE P amefanikiwa  kutoa  salamu zake  za  mwisho  kwa  rafiki yake  kipenzi  ambaye  alikuwa  naye  huko  Afrika  kusini  tena  walikuwa  ndani  ya  chumba  kimoja  kabla ya  mauti  kumkuta Ngwea....!!
Mwanzoni, M 2 THE P alikuwa  amefichwa  na  kudanganywa  kuwa  Ngwea  alikuwa  ametangulia  Tanzania. Baadaye  Maggie  alilazimika  kumweleza  ukweli......